Muigizaji wa Filamu nchini Burundi Mr Ernest ni kijana anaejituma sana kwenye Tasnia ya Burundi.
Baada ya kutowa movies zilizowafurahisha mashabiki wa filamu, amekuwa kimya bila kutowa kazi takribani miezi 6 na katika maongezi yake na Indundi tumemuuliza kwanini yuko kimya kiasi kwamba hasikiki kwenye Movie ame sema :
«Mimi nimejifunza mambo mengi sana kuhusu sanaa ya nyumbani Burundi ila kitu ambacho nimegunduwa kwanza ni kwa wale wasanii waliotutangulia hakuna msaada wowote wanao tusaidia sisi kwa kutuonesha njia nzuri ya kufuka mahali walipo ila watambuwe jambo tukiwa sote kwa umoja lazima tufike mbali maana sanaa ya Burundi bado inaitaji ushirikiano mkubwa na ikiwa tutaishi ivi bila kushirikiana kwa kweli itakuwa bure sana ndio maana naomba kwa wasanii tupendane na tushirikiane kwa umoja.
Jambo lapili naweza kusema kwamba Filamu ya Burundi tunakwama kwa kweli yote ni kwasababu hatuna sapoti tunaitaji kupata sapoti ili tuweze kuinuwa Tasnia yetu ya Filamu maana kwa sisi vijana kweli tunajituma tunaomba serikali iweze kutusaidia ili tufike mbali.
Na kuhusu ukimya wangu katika miezi sita kweli nimejifunza mambo mengi sana na niseme tu kwamba lazima nifanye kazi nzuri mwaka huu ambayo itakuwa pendezo kwa watu wote. »
Umoja wa wasanii walioendelea wakishirikiana pamoja na walio nyuma yao lazima watafikia malengo yao.