BurundihomepageIndundi CinemaMoviesswahili

Producer wa Filamu nchini Burundi POPS anarudi upya


Producer wa filamu nchini Burundi kwa jina la Muhirwa Olivier maarufu kama Pops ni kijana mtengenezaji wa nyimbo za wa Star wengi pia ni Mtengenezaji wa Filam.

Hapo ni baada ya kusimamisha kazi za filamu mwaka 2018 hadi sasa kutoonekana kwenye Game ,na maamzi yake kwa sasa ameamuwa kurudi kwenye Game ya Filamu basi tuliweza kumtafuta nakuzungumza mawili matatu alifunguka na kusema :

Kusema kweli ni mda mrefu sana sipo kwenye Game ya Filamu nchini na yote imetokana na kuwa busy mda mrefu kwa sababu nimeona kwamba Filamu za Burundi hazilipi na hazina mwanga wowote ule,ndipo nikaamuwa zangu kuanza Clip Video na kweli nikaona zinaingiza, ila nazidi kuona kama ili Filamu za Burundi ziendelee lazima pia nasisi tuwwze kuchangia ,ndio maana kwa sasa nimeamuwa kurudi kwenye Game na mwezi wa nne mtaanza kuona kazi zangu na zenye ubora zaidi na zenye mabadiliko. Pia nikumbushe tu warundi kwamba ili Filamu ziendelee lazima tupende vya kwetu sana ili kusaidia vijana wetu’’. Alimaliza Pops.

Kweli katika muonekano wakazi zake Pops ni kijana ambae anajituma sana kwenye kazi ata ukitazama kazi zake anazotengeneza zina Quality nzuri ,na yote inaesabika kwenye Movie ili iwe nzuri lazima image na sound viwe na ubora mkubwa.

What's your reaction?

Related Posts

1 of 717