BurundihomepageIndundi CinemaMoviesswahili

Msanii wa kike anaetamba na filamu yake ya House Girl aja upya

Migizaji wa Filamu nchini Burundi maarufu Huguete anazidi kuonekana na ubora mkubwa sana kwenye kazi zake za filamu hadi kujichukulia umaarufu mkubwa sana kwenye Tasnia ya Filamu Burundi, hapo mwanzo mwana dada uyo alikuwa akifanya kazi bila kuonekana na iyo hali ilitokea kumsumbuwa sana kabisa hadi kukata kitumaini chakuendelesha kazi ila baada ya hapo alikuja kuonekana mara moja kwenye kazi ya House Girl ndipo alionesha uwezo wake mkubwa na Kukubalika, na tulipo zungumza nae amesema :

Kusema ukweli nimekaa mda mrefu sana nakuona sina mataa yakuendeleza maana kila kazi nilikuwa nikijaribu kutengeneza nimekuwa nashindwa kufikia malengo, maana tokea nianze Filamu sasa nina miaka zaidi ya tano (5) ila sioni mafaa yoyote kabisa ,nikaamuwa kuachana navyo,ila Baada yakupata shauri mbali Mbali niliamuwa kurudi na nikatumika Filamu ya HOUSE GIRL Kweli ni Filamu ambayo imeweza kunitowa na naona jina langu kurudi tena nakupendwa na kila mtu,ndio maana nitowe neno tu moja kwa shabiki zangu ni kwamba kwasasa nakuja upya kabisa na wasubiri Filamu zangu zingine ambazo zinakuja ni nzuri sana kabisa,Pia naomba washabiki wangu wazidi kunisapoti sana’’. Alimaliza ivo.

Kweli ni msichana anae zidi kufanya vizuri siku kwa siku, na kwasasa aja na muonekano mpya kwa kweli,Mungu azidi sana kusaidia waigizaji wa Filamu Burundi, na tuzidi kuwasapoti vijana wetu.

What's your reaction?

Related Posts

1 of 717