homepageIndundi CinemaMoviesswahili

Jaden Vicky : “Acheni uzushi kwenye kazi ya filamu”

Muigizaji wa Filamu nchini Burundi Jaden Vicky maarufu kwa jina la JADEN ni muigizaji mzuri wa filamu nchini Burundi na anaonekana mwenye kujituma kwa nafasi yake kuakikisha kwamba anaweza kurizisha washabiki wake wote kwa ujumla.

Na Baada yakumuona kwenye Filamu iitwayo DHAMIRA CHAFU, basi Indundi imeweza kumuuliza ni kwanini amesema kwamba wanaume waache uzushi kwenye kazi alijibu kwamba:

“Ukweli unasemwa waigizaji wengi wa Filamu nchini Burundi wako kama hawako kazi yao wamebaki kuwa nyuma ya wanawake tu kwa hio waache mambo yakizushi nawajikaze tupige kazi ili tuweze kupandisha hatuwa ya nchi, inabidi tujifunze na tujiulize kwanini Tanzania wanazidi kuendelea yote ni kwasababu wanajituma, hakuna Media inaweza kusaidia msanii asiye jielewa, Kweli Burundi mwaka huu tunatakiwa kupata star ambaye atatuwakilisha sisi kimataifa nasiyo kimasiara na nikumbushe tu watu kwamba Soon naachia Movie inaitwa DHAMIRA CHAFU ,Kweli niseme asanteni sana kwa mapokezi ya Trailer kweli Mungu azidi kuwa bariki na niwaambie tu kwamba mwaka huu lazima nitaakikisha natumika kwa kasi kubwa kiasi kwamba nifunuwe watu macho,acha nimalizie apa ila mengi zaidi mtajuwa”. Alimaliza Jaden…

Tasnia ya Filamu Burundi inaitaji upendo na ushirikiano mkubwa ili wasanii muweze kufikia kupiga Hatuwa kubwa mwaka huu maana Kwenye kazi pakiwa Umoja lazima nguvu ionekane kwa sana.

Towa Maoni yako juu ya kitu alicho kiongea Jaden.

What's your reaction?

Related Posts

1 of 688