homepageCECAFA Challenge cupIndundi CinemaMoviesswahili

Kabizi le Comedien kurudi kwenye game ya Comedy kitofauti

Kabizi ambae nikijana mchekeshaji kwenye Tasnia ya Filamu Burundi anae fahamika kama Kabizi l’eau comedien kama anavyo jiita, pia amefanya kazi kubwa nakuweza kujipatia umaarufu kwenye kazi yake pia na mashabiki siku kwa siku kwa video anazozifanya hadi kuanza ku perform kwenye ma stage COMEDY STEND UP na kuchekesha watu.

Basi tulipokutana naye na tukamuuliza kwa ukimya wake mda mrefu, alisema:

“Mimi kwanza najiamini na naelewa kila kitu ninacho kifanya kwa hiyo ukimya wangu haukuwa kama watu wanavyo fikiria ila umekuwa wakujipanga nakuona jinsi Comedy nchini Burundi tumeichukulia kama mtaani yaani ili watu waweze kuonekana kwenye whastApp na wapate umaarufu ila sisi comedy tunaichukulia kama kazi na njia moja ya kutupa sisi maisha ya baadae.” Alisema Kabizi.

Basi alipoulizwa sasa nini anacho fikiria kwa mapinduzi amesema kuwa :

“Baada ya ukimya wangu sasa nimekuja na kazi hii ila niseme tu kwamba nakuja kitofauti sana na kazi za hali ya juu sana kwa kweli, ila kama ombi naitaji watu wanao towa video za comedy ambazo hazieleweki waache na watutafute tusaidiane ili waweze kuwa bora na sio kila video wanatowa eti ni comedy baadae mashabiki wanaanza kusema kwamba Burundi akuna Comedy please waache mambo kama hayo.”
Alimalizia ivo Kabizi.

Kama tunavyojuwa Kabizi ameanza kama mtani ila leo anaonekana ni kijana anayependwa zaidi sanaa.

What's your reaction?

Related Posts

1 of 688