BurundihomepageIndundi CinemaMoviesswahili

Mzungu muigizaji wa filamu Gitega na ujio wa Filamu mpya

Mchezaji wa Filamu nchini Burundi maarufu kwa jina la Mzungu nwenye makaazi yake mkoani Gitega baada ya kufanya interview na Indundi Tv kwa sasa anakujia bonge la kazi ambayo anatarajia kwa mda siyo mrefu kuachia kazi hiyo, na uku akionekana mwenye kuomba misaada mbali mbali ili aweze kufanikisha swala la uzinduzi ili apate jinsi yakuweza kufikisha kazi yake kwa washabiki wake. Baada yakuona cover hiyo tumeweza kuwasiliana naye na tukaongea kuhusu kazi yake ameweza kusema :

“Kweli mimi nakosa uwezo wakunifikisha pale ambapo ninapo paitaji mimi ,maana nina shida kweli yakufikisha kazi yangu mbali tofauti na hapa nilipo leo,na unajuwa kwamba kweli Burundi tunaweza sana kuigiza natunajuwa Filamu ila kama leo tunashindwa kufikia pale ambapo wengine wanapo fika ni kwa sababu sisi hatuna sapoti kama zile ambazo wao wako nazo. Ila tu mimi naamini kwamba mambo yatakuwa mazuri sana ikiwa tutapata sapoti na sisi pia. Kitu kingine ambacho nikama ombi kwa kweli ninakazi ambayo napangilia kuachia siku za usoni ni filamu ambayo nimesimamia mimi na kundi langu na kuonesha nguvu zetu, ila kwa sasa nipo kwenye harakati zakutaka kuachia kazi hiyo. Kweli naomba sapoti kwenu muweze kunisaidia ili niweze kufika mbali, tambuweni vijana wenu wanaweza inabidi kuwaunga mkono. Pia nasema na wasanii wa Bujumbura tuweni pamoja na tuweze kusaidiana kabisa.”. Alimaliza Mzungu.

Kweli kundi hili la huyu kijana linazidi kufanya vizuri kwenye mkoa wa Gitega, maana anaonekana ni kijana mwenye kujituma kwa kutengeneza Filamu za Kiswahili pia na Filamu za Kirundi, kweli Mungu aweze kukujalia ili aweze kufika mbali.

What's your reaction?

Related Posts

1 of 717