homepageCECAFA Challenge cupIndundi CinemaMoviesswahili

Salumu Jimmy na Filamu yake mpya “mda mhafaka”

Kijana mwenye uwezo mkubwa wakuigiza ajulikanae kwa jina la Salumu anaendelea kufanya vizuri siku baada ya siku nakuitaji kuleta maendeleo kwenye company yake ya SALUMU THE FUTURE FILMS na kwa sasa anaitaji kuachia filamu yake mpya. Pia ameelezea Indundi Tv akisema :

“Mimi nina miaka mingi sana kwenye hii kazi pia najaribu kujituma siku baada ya siku ili kuweza kujaribu kupinduwa tabia ambazo zilizopo na zinazo sababisha filamu za nyumbani kutoendelea kabisa niseme tu kwamba najitaidi kufanya mambo mazuri pia naamini nitafika na ndio maana kwenye Filamu yangu ya MDA MHAFAKA nimetumia wasanii wakubwa wa Buja Movie pia wenye uwezo mkubwa wa kuigiza pia na wasanii wangu waliopo ndani ya SALUMU THE FUTURE FILMS waliweza kunioneha uwezo mkubwa sana wa kuigiza pia nishukuru sana na Director aliesimamia filamu hii, na niseme jambo kwa viombo vya habari kweli wajitowe sana kutusaidia maana sisi bila wao hatutafika popote. Kwa hio umoja ni nguvu wajuwe tu kwamba tunaitaji nguvu yao kwa kweli na naamini tutafika.

Pia Indundi asanteni sana kwa kutujali kwa njia zote sanaa ya filamu inaitaji msaada kwa viombo vya habari mkijitokeza na kusaidia ku promote kazi zao ili waweze kufika mbali najuwa kwa umoja na pamoja lazima tutafika kwa bidii pia ambayo waigizaji wa filamu wanazidi kuonesha”.

What's your reaction?

Related Posts

1 of 688