homepageCECAFA Challenge cupIndundi CinemaMoviesswahili

Shabani, msanii wa filamu za Burundi na ndoto kubwa

Msanii Shabani maarufu kama Shablix ni mkurugenzi wa Company ya LA COLOMBE BLANCHE ambayo kwa sasa ina zaidi ya miaka 8 kwenye game nakufanikiwa kufanya movie zakutosha ila mbali na yote movie yake ya PENZI LA JENITA ndo imekuwa movie kubwa sana kutengenezwa Burundi ndani yake unaona kuchezea katika uwanja wa ndege na ilishangaza sana wasanii wenzake kwa mara ya kwanza kuonekana katika tasnia ya Filamu za Kiswahili hapa nchini Burundi.

Basi Indundi kama kawaida kwa maendeleo ya vijana imezungumza naye nakumuuliza nini anacho kipanga Shabani alisema :

“Kwanza kutokana na swali lenu mkisema ninavyo jipanga mnakosea ila mniulize nini naandaa maana saa izi naandaa kazi kubwa sana ambayo itakuja na utofauti mkubwa sana kwenye game yetu kweli nimefanya filamu ya PENZI LA JENITA na nimefanya uzinduzi kwenye ukumbi wa Palais des Arts na watu wamekuja kuitikia na nimeshukuru sana kwa kweli maana ni moja ya amendeleo pia baada ya kazi hio kwa sasa naandaa kuachia kazi ambayo kila mtu akiona atasema ndio, na kitu kingine nazidi kufurahi sana maana game ya nyumbani inaanza kubadilika na maendeleo tunaanza kuyaona kwa iyo nikujitaidi tuwe wabunifu wa hali ya juu maana Burundi sisi tunaweza sanaa“. Alimaliza Shabani

Burundi wasanii wakiamka na kuleta mapinduzi makubwa kwenye game hii maana huwezi kufanya jambo ukiwa kitandani usingizi ndo unakakutawala ila ukijitowa kwa hali ya kusimama lazima utafika.

What's your reaction?

Related Posts

1 of 688