homepageIndundi CinemaMoviesswahili

Yvonne : «Nimekuwa nimeacha Filamu kwa mda mrefu ila now narudi »

Muigizaji wa Filamu nchini Burundi kwa Jina la Belyse maarufu Kama Yvonne, hapo ni baada ya kuacha Filamu kwa mwaka mzima na ni msichana mwenye uwezo wakuigiza Filamu zake na alikuwa akizitumika kwa kujituma na hadi kufanikisha kushiriki kwenye Filamu nyingi kama THINK BEFORE YOU ACT, JENEZA LA MAMA na zingine tofauti ,na aliweza kusimamisha Filamu kwa mwaka mzima na kwa sasa kuamuwa tena kurudi kwenye Game. Basi hapo ni baada ya sisi kuwasiliana naye kutokana na ukimya wake ndo akafunguka akisema :
«Kusema ukweli nimekuwa nimeacha Filamu kwa mwaka mzima sasa na hapo imekuwa imesababishwa na maisha maana nilipo kuwa naigiza nimekuja kugunduwa kwamba Filamu pia inaitaji gharama na bila kipato kabisa ni bule pia kuchangia maisha mimi ni mwanamke nastaili kuwa na muonekano kama mwanamke Muigizaji kama tunavyoona wasanii wenzetu wa nchi jirani, so iyo ndo ikanifanya kabisa niwe busy kwa ajili ya kutafuta maisha uku na kule ila naamini kwa sasa nimejipanga vya kutosha na narudi kazini kwa bidii kubwa ,najuwa nimepoteza washabiki wangu na wengine kukosa kazi zangu ila niseme tu kwamba soon tu nitaachia kazi maana kwa sasa nipo najiaanda kufanya kazi kubwa, na asante sana Indundi Tv kuwa karibu na sisi waigizaji. » Alimaliza YVONNE.

Mafanikio na kipato hutafutwa na sisi wenyewe ,Indundi Tv iko karibu na wasanii na kuwasaidia kusambaza kazi zao na kuwatangaza siku kwa siku.

What's your reaction?

Related Posts

1 of 688