BurundihomepageIndundi CinemaMoviesswahili

Itangishaka Julien: Narudi kwenye game ya filamu ili nipambane na wenzangu

Muigizaji wa Filamu nchini Burundi aitwaye Itangishaka Julien aonekana na utofuti mkubwa sana kwenye kazi zake, ni mda mlefu sana kijana huyo apatikani kabisa kwenye Game yoyote ile ya Filamu kutokana na hali nyingine ya maisha, na ukitazama ni kijana mwenye uwezo mkubwa sana wa kuigiza ,na ameweza kushiriki pia kwenye Movie moja na msanii aliye kuwa Maarufu nchini aitwaye Mkombozi ndani ya Filamu iitwayo REVENGE na aliweza kuonesha uwezo mkubwa na hapo alicheza kama jambazi ,na filamu hiyo imeweza kujipatia umaarufu mkubwa sana nchini, na baada ya hapo alifanya Filamu zingine 3, ARDHI YA CHOKWE,CHOZI LA MAMA na FIKRA. Basi alipotangaza kwamba anarudi kwenye uigizaji tena ndipo tulimtafuta na kuongea nae aliweza kufunguka na kusema:

«Kusema ukweli kwanza namshukuru Mungu sana kwakuweza kunipa uhai ,pili nashukuru sana nyinyi Watangazaji wa Indundi Tv kwa vile mnavyo jitowa kuweza kutusaidia kweli Mungu awabariki sana tena sana maana ni hatua mnayozidi kutupigisha. Basi nikisema kuhusu Mimi, ni kweli nimekuwa nimesimamisha game kwa mda wa miaka 2 sasa ,ila nimeamuwa kurudi baada yakuona kwamba sijatenda haki kutupa kazi ambayo itakuja kueshimisha inchi yetu wenyewe,Basi nimeamuwa kurudi na kupambana na kazi hii, kweli akuna ahadi nitakayo itowa kwa wale washabiki wangu ila tu niwaambie kwamba wasubiri wataona matokeo. »

Itangishaka alizidi kufanya vizuri kwenye kazi ila kwa maneno yake kipindi alipokuwa anaongea inaonekana wazi kwamba kuna kitu anacho kiogopa kama kutowa ahadi yoyote kwa watu wake kutokana na kipindi kirefu hayupo tena kwenye Game.

 

What's your reaction?

Related Posts

1 of 702